DAMU SALAMA

Posted on: May 5th, 2024

KITENGO CHA DAMU SALAMA

Kitengo cha Damu salama  hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani-Tumbi kilianzishwa rasmi mwaka……………..Kitengo hiki kipo chini ya maabara kuu ya hospitali ya mkoa wa Pwani-Tumbi na kinashughulikia maswala ya utoaji  wa huduma ya damu salama kwa wahitaji wa damu ndani na nje ya hospital kwa kushirikiana na damu salama makao makuu kwa  kufuata (Standards Operating  Procedures -SOP)  kwa ajili ya kuhakikisha  mgonjwa  anapata damu iliyo salama.

Hospitali ya Tumbi ina uhitaji mkubwa sana wa damu kutokana  na  wahanga wa ajali ukizingatia hospitali yetu ipo kando kando ya barabara kuu ya morogoro pia uhitaji upo kwa  wagonjwa wengine toka sehemu mbalimbali . Kwa sasa kituo kinakusanya chupa  12-18  kwa  siku ,  60kwa wiki , 240 kwa mwezi wastani wa chupa 13 kwa  siku sawa na chupa 65 waq wiki sawa na  chupa 260 kwa mwezi. Kwa kiasi hiki kinakidhi mahitaji ila tunatakiwa kuongeza nguvu zaidi ili tuwe na akiba ya damu ya kutosha.  Wadau wakuu wa uchangiaji damu ni wanafuzi, taasisi za dini,,majeshi na ndugu wa mgonjwa.

SHUGHULI ZA KITENGO

  • Kusimamia na kuhakikisha usalama wa damu kwa wagonjwa
  • Upatikanaji endelevu wa damu salama hospitalini
  • Uchangiaji wa  wa damu wa kila siku ndani ya kitengo.(walk-in donors)
  • Utafutaji wa maeneo salama  ya uchangiaji damu-( mashuleni, Vyuoni, makambini ,na kwenye jamii.)
  • Upokeaji na Urudishaji wa majibu kwa waliochangia damu.
  • Kutoa elimu sahihi kuhusu uchangiaji wa damu na  kuhimiza umuhimu wa  kupima afya kupitia kuchangia damu
  • Unasihi  wa ndugu wa mgonjwa na wachangiaji damu salama


Kitengo cha damu salama  kinahitaji ushirikishwaji wa  wadau mbalimbali wa  kuchangia kwa hali na mali ili  kupunguzia  serikali mzigo