MAFUNZO YA UFUATILIAJI NA TATHMINI (MONITORING AND EVALUATION) TUMBI

Posted on: October 23rd, 2025

Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi, wamepata mafunzo ya Ufuatiliaji na Tathmini (Monitoring and Evaluation) yaliyoanza tarehe 20 Oktoba 2025 mpaka leo tarehe 24 Oktoba 2025,  kwa lengo la kuwajengea uwezo kwenye kutekeleza majukumu yao ya kazi za kila siku.

Mafunzo haya yameandaliwa na uongozi wa hospitali kwa kushirikiana na wawezeshaji kutoka  Wizara ya Afya  ambao ni Ndg. Kiiza Kilwanila, Bi. Mwahija Hamisi, na Ndg. Andrea Ibrahimu.