Utawala

2.1. Uongozi na Utawala

Utoaji wa huduma bora utategemea misingi ya uongozi na utawala inayozingatia sheria, taratibu na

kanuni. Misingi hiyo itajumuisha uwajibikaji, usawa, uwazi na ushirikishwaji wa wadau wote katika

utoaji wa huduma za afya ikiwemo uwepo wa Bodi ya Hospitali inayowajibika ipasavyo.

Ili kuhakikisha utekelezaji wake unafanyika kwa uwazi: -

 Menejimenti ya Hospitali inatakiwa: kufanya vikao kama ilivyoelekezwa kwenye miongozo

iliyotolewa na wizara; kutoa tarifa kwa mamlaka husika; kupokea maoni/malalamiko ya wateja

na watoa huduma na kuyafanyia kazi;

 Kila Hospitali inatakiwa kuwa na utaratibu wa kutoa mrejesho kwa wadau wote kuhusu hatua

zilizofikiwa juu ya kushughulikia changamoto za uendeshaji wa Hospitali na utoaji wa huduma

za afya.

2.2. Rasilimali Watu katika Hospitali za Rufaa za Mikoa

Rasilimali watu katika Hospitali za Rufaa za Mikoa ni mojawapo ya nyenzo muhimu katika kutoa

huduma bora za afya. Serikali imefanya jitihada katika kuboresha rasilimali hii kwa njia mbalimbali,

ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya wataalamu, kuboresha ujuzi katika nyanja mbalimbali, kuongeza

mishahara na maslahi mengine kwa watumishi. Pamoja na jitihada hizi, kuna changamoto kadhaa

zitokanazo na rasilimali watu zinazoathiri utoaji wa huduma za afya: -

 upungufu wa watumishi/wataalamu katika hospital za Rufaa za mikoa,

 uwiano wa ujuzi, usiokidhi (idadi ya wataalamu dhidi ya idadi ya watu) kulingana na ikama.

Sanjari na changamoto hizi, Wizara itaendelea kuwapanga watumishi waliopo kwa uwiano sahihi

katika Hospitali zote 28 za Rufaa za Mikoa. Aidha, usimamizi wa watumishi unatakiwa kuzingatia

sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa umma zilizoidhinishwa na mamlaka husika. Hivyo: -

 Timu ya Menejimenti ya Hospitali inatakiwa kushiriki kikamilifu kwenye uandaaji wa makisio ya

bajeti za mishahara ya watumishi kulingana na mwongozo wa Ikama na kuwasilisha kwa Katibu

Mkuu kila mwaka wa fedha;

 Uongozi wa Hospitali unatakiwa kuhahikisha unasimamia watumishi waliopo kwenye maeneo

yao husika ili kuwezesha utoaji wa huduma bora kwa viwango vinavyokubalika;

 Kusimamia utoaji maslahi na haki mbalimbali za kiutumishi;